Victim photo

Abdallah Saad Hussein

Hali: Aliuwawa Umri: 31

Wasifu:

Alikuwa ni mwalimu wa madrasa msikiti wa Qadiria (Maarufu kwa Sheikh kishki) kwa Mathias Kibaha. Alikuwa ni kijana mpole na asiye na mambo mengi. Na alijukikana Sana maeneo Yale ya kibaha kwa Mathias

Alipoonekana mwisho: Pwani

Aliuwawa kwa kupigwa risasi na polisi siku ya tarehe 30/10/2025 akivuka barabara kwenda kuswali swala ya saa 7. Mwili wake ulihifadhiwa Tumbi hospital kwa siku kadhaa kabla ya kwenda kuzikwa Turiani-Morogoro nyumbani kwa baba yake.